Duration 4:47

Chips Za Muhogo/How to make cassava chips or chakri

6 222 watched
0
65
Published 24 Apr 2020

...Chipsi Za Muhogo... By Laylunnar Mo ...Mahitaji... Muhogo fresh kiasi utakacho Pilipili ya unga upendavo Chumvi kiasi Ndimu ya unga kidogo Njugu za maganda upendavo Mafuta ya kukaangia ...Mataarisho... Menya maganda muhogo wako wote Kisha ufute uzuri kwa tissue au kitambaa (usikoshe) Chukua cha kuparia sehemu kubwa upare muhogo wako wote Kisha tandaza uzuri kwenye sahani Kama muhogo wako una maji na uko nchi za joto basi uanike kidgo tu usikauke kabisa Au ukamue kidgo tu sio sana utavunjika Kama hauna maji basi weka mafuta yako moto wa kiasi uanze kukaanga mpaka rangi upendayo uzitoe, kaanga zote umalize Punguza moto ukaange njugu zako umalize Wacha vote kwa tissue vitoke mafuta Kwenye bakuli kubwa vunja vunja chips zako tartibu usivuruge, mimina njugu,chumvi, pilipili na ndimu ya unga kisha zipete uzuri na ukoroge na mwiko Onja kuhakikisha zimekolea, kisha zihifadhi uzuri kwa bakuli la ufuniko au ziweke kwenye freezer bags. Kula kwa mbatata, kwa chatne au chakua tu. By Laylunnar Mo By Laymoz's Zenji Delicacies Kidokezo! Ukitumia fryer hakikisha usiweke basket yako mpaka chini ukisha weka muhogo sababu mafuta yatapanda juu, zuia kwanza kwa juu yakisha pungua kasi utaiwacha chini, hii husababishwa na maji ya muhogo na starch yake. 🍲Enjoy

Category

Show more

Comments - 3